Thursday, 20 November 2014

KUHUSU MTOTO KUFARIKI KATIKA AJALI MAHAKAMANI HUKO UGANDA


 


Mtoto wa mwanamke mmoja amefariki wakati mama yake alikuwa anapandishwa kizimbani baada ya kukamatwa akiuza bidhaa barabarani kinyume na Sheria.
Mtoto mwenye umri wa miaka miwili amegongwa na gari na kufa katika Makao Makuu ya Halmashauri ya jiji la Kampala KCCA, ambapo mama yake Madina Namakula alifikishwa Mahakamani Kampala, Uganda, kusomewa shitaka lake ambapo wakiwa Mahakamani hapo ndipo mtoto huyo alipopata ajali hiyo.
Kwa mujibu wa mashuhuda wamesema kuwa Polisi wamesababisha kifo cha mtoto huyo.
Mtoto huyo amezikwa leo Kampala, Uganda.

Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook

0 comments:

Post a Comment