Friday, 28 November 2014

PENNY AFUNGUKA: SIWEZI KUVUNJA USHOSTI WA WEMA, AUNT!



Stori: IMELDA MTEMA

MTANGAZAJI Bongo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuwagombanisha marafiki wa damu, Wema Sepetu ‘Madam’ na Aunt Ezekiel, baada ya yeye kuingilia urafiki huo.Mtangazaji Bongo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ akiwa na Wema Sepetu.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Penny alisema kuwa anaamini kabisa kuna baadhi ya watu hawapendi kuwa na urafiki zaidi ya watu watatu kitu ambacho siyo sahihi, yeye anaamini baada ya kupatana na Wema hivi karibuni, watakuwa marafiki watatu.

Wema Sepetu akiwa na Aunty Ezekiel.

“Nafurahi sana tunapokuwa na kampani kubwa nashangaa wengine mpaka wanafikia kupigana kisa akiona rafiki yake ana urafiki na mtu mwingine, mimi napenda tuwe wengi ili tuweze kushauriana mambo mbalimbali,” alisema Penny.

Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook

0 comments:

Post a Comment