Nida,
(1949). Kama alivyonukuliwa na Mgullu, mofu ni umbo la neno ambalo
huwakilisha mofimu na ambalo hudhihirika kifonolojia na kiothografia.
Mofimu ambazo ni elementi dhahania huwakilishwa na mofu ambazo
hudhihirika ama kifonolojia zikiwa ni sauti za kutamkwa au
kiothografia zikiwa ni alama za kuandikwa.
Hivyo
basi, mofu ni kipashio cha kimofolojia kiwakilishacho mofimu.
Kwa
kuzingatia ufafanuzi huu, ni wazi kabisa zinaelezea mambo ya msingi
kuhusu sifa muhimu zinazopambanua dhana ya mofu. Sifa hizo ni pamoja
na:
Mofu
ni sehemu halisi ya neno. Ni wazi kuwa, mofu ni maumbo halisi ya
maneno ambayo hutamkwa wakati watu wanapozungumza au kuandikwa wakati
watu wanapoyaandika (Mgullu, 1999).
Mofu
hudhihirika kifonolojia na kiothografia. Kutokana na kuwa mofu ni
umbo halisi la neno, basi mofu mbalimbali hudhihirika kifonoljia
zinapotamkwa na pia kimaandishi zinapoandikwa (Mgullu, 1999).
Mofu
huwakilisha maana. Msisitizo hapa ni kwamba, mofu huwakilisha maana.
Kwa hiyo, katika neno lolote katika lugha yeyote panakuwepo maana na
maana hizo huwa zimesetiriwa katika mofu zilizopo katika neno. Hata
hivyo, kuna maneno mengine ambayo hayana mofu. Kwa mfano, maneno kama
vile Baba, Mama na Kaka. Maneno haya ni huru hivyo hayawezi
kugawanyika zaidi (Mgullu, 1999).
Mofu
ni kipashio kidogo kabisa cha neno chenye maana. Hapa kinachotiliwa
mkazo ni ule ukweli ya kuwa mofu ni sehemu ndogo kabisa ambayo hubeba
maana na kwamba sehemu hiyo haiwezi kugawanywa katika sehemu ndogo
zaidi zilizo na maana (Mgullu, 1999).
Bauer,
(1983). Kama alivyonukuliwa na Mgullu, alomofu ni mofu mojawapo
katika seti ya mofu zinazowakilisha mofimu fulani ambayo ina
mazingira yake ya kifonetiki, kileksika au kisintaksia.
Ufafanuzi
huu unaelezea sifa muhimu zinazoifafanua alomofu. Sifa hizo ni pamoja
na alomofu ni umbo, ambapo ni umbo halisi ambalo ni sehemu ya neno
fulani na ambalo hutamkwa na kuandikwa. Alomofu ni mofu mojawapo
miongoni mwa mofu za mofimu moja. Tofauti inayojitokeza hapa ni kuwa
mofu huwa ni mofu wakati ambapo umbo moja tu hutumika kuiwakilisha
mofimu fulani (Karanja, 2004).
Kwa
hiyo, alomofu ni umbo mojawapo kati ya maumbo kadhaa tofauti
yanayowakilisha mofimu moja.
Ufuatao
ni ufafanuzi wa mofu au alomofu zilizo katika maneno yafuatayo na
aina zake:
Mamake.
{mamake}- ni umbo la
nje.
{mama} {yake}- ni
umbo la ndani.
Kwa
hiyo, neno mamake lina mofu mbili, yaani {mama} na {yake} ambapo,
{mama} ni mofu huru na {yake} ni mofu changamano, lakini mofu {ke} ni
mzizi tegemezi, kwa sababu {ya} inaweza kubadilika. Kwa mfano, zake.
Kuta.
Neno
kuta lina mofu mbili, yaani {Ø} kapa na {kuta}.
Mofu ya kwanza ni
kapa {Ø}.
Mofu {kuta} ni mzizi
funge.
Chezea.
Katika neno hili
kuna mofu tatu, yaani {chez}, {e} na {a}.
{chez-} ni mzizi
tegemezi wa kitenzi.
{-e-} ni alomofu
tegemezi na tata ambayo inaleta dhana ya kutendea.
{-a} ni alomofu
tegemezi ambayo ni kiambishi tamati yakinishi.
Wanahewa.
Neno
hili lina mofu mbili, yaani {w} na {anahewa} ambapo,
{w} ni
mofu tegemezi, wakati
{anahewa}
ni mofu changamano ambayo imeundwa na mizizi miwili, yaani {ana} na
{hewa}.
Mwanagenzi.
{mwanagenzi}- ni
umbo la nje, wakati.
{muanagenzi}- ni
umbo la ndani.
Neno
hili lina mofu mbili yaani, {mu}- ni mofu tegemezi na mofu
{anagenzi}- ni mofu changamano ambayo imeundwa na mizizi miwili
ambayo ni {ana} na {genzi}.
Hivyo
basi, ili kupambanua dhana ya mofu au alomofu, inakupasa utambue sifa
zinazopambanua dhana hizi mbili, lakini pia uweze kutambua umbo la
nje na la ndani la neno husika ili kuweza kubainisha vema mofu au
alomofu zake zinazounda neno husika.
MAREJEO
Habwe,
J na Karanja, P (2004). Misingi
ya Sarufi ya Kiswahili.
Nairobi: Phoenix Publishers
Mgullu,
R. S (1999). Mtalaa
wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili.
Dar es
Salaam:
Longhorns Publishers.
Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook
0 comments:
Post a Comment