Thursday, 11 September 2014

EBUUUUUUU ONA HII RAIS KIKWETE, MUSEVENI WALONGA FARAGHA KWA ZAIDI YA SAA MOJA IKULU




THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatano, Septemba 10, 2014, amefanya mazungumzo ya faragha na mgeni wake, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Ikulu, Dar Es salaam.
Rais museveni ambaye alikuwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika Tanzania, aliwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kiasi cha saa 4 na dakika 10 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais Kikwete.
Mazungumzo kati ya viongozi hao wawili, yalianza saa tano unusu asubuhi na kuchukua kiasi cha saa moja na dakika 15.
Rais Museveni aliondoka Ikulu baada ya chakula cha mchana na aliagana na mwenyeji wake, Rais Kikwete kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar Es salaam, kabla ya kupanda ndege yake kurejea nyumbani.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
10 Septemba , 2014.

 ANKO SAM

Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook

0 comments:

Post a Comment