Waandishi wa habari wakirekodi tukio la kuwasili kwa Mh. Freeman Mbowe (hayuko pichani) Makao Makuu ya Polisi.
MNYIKA, WANASHERIA WAZUIWA KUINGIA NDANI WANAHABARI WAKIMBIZWA NA MBWA, WAUMIA, WAMWAGA MACHOZI
MAMIA ya watu wamejitokeza leo kumsindikiza Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, baada ya kuhitajiwa kufika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, jijini Dar es Salaam kuhusiana na kauli yake aliyotoa majuzi juu ya kuitisha maandamano nchi nzima kupinga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba.
Kilichofuata ni polisi kuamuru watu wote waondoke eneo hilo kwa umbali wa mita 200 ambapo walikimbizwa na mbwa wa polisi na kusababisha wengi wao waumie na kupoteza vitu vyao mbalimbali, hususani wanahabari ambao baadhi yao waliumia na kupoteza zana zao za kazi.
ANKO SAM BLOG
Like Page Yetu Hapa Kuungana Nasi Facebook
0 comments:
Post a Comment